1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu awashtumu waliolitambua taifa la Palestina

26 Septemba 2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, leo ameyashtumu vikali mataifa ya Magharibi kwa kulitambua taifa la Palestina.

Israel Jerusalem 2025 | Benjamin Netanjahu
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin NetanyahuPicha: Amos Ben Gershom/Israel Gpo/ZUMA/picture alliance

Akilihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kiongozi huyo wa Israel alishtumu hatua za kidiplomasia za washirika wakuu wa Marekani zinazozidisha kutengwa kimataifa kwaIsraeli kwa hatua zake katika vita na kundi la wanamgambo la Hamas.

Netanyahu ameongeza kuwa, viongozi wa Ufaransa, Uingereza, Australia, Canada na mataifa mengine yalilitambua taifa la Palestina baada ya mambo ya kutisha yaliofanywa na Hamas mnamo Oktoba 7, mambo anayodai yalipongezwa na asilimia 90 ya Wapalestina.

Kiongozi huyo pia amesema viongozi wengi wanaomshtumu hadharani wanampongeza faraghani.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW