1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu kufanya mazungumzo na Trump Washington

11 Februari 2026

Rais wa Marekani Donald Trump atakuwa mwenyeji wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu leo.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na Rais Donald Trump wa Marekani
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na Rais Donald Trump wa MarekaniPicha: Jonathan Ernst/REUTERS

Kulingana na Netanyahu, mazungumzo yake na Trump katika ikulu ya White House yatajikita katika mazungumzo ya Marekani na Iran.

Waziri mkuu huyo wa Israel amesema atauwasilisha mtazamo wa Israel katika mazungumzo hayo na Jamhuri hiiyo ya Kiislamu.

Viongozi hao wawili pia wataijadili hali katika Ukanda wa Gaza na eneo zima la Mashariki ya Kati.

Gazeti moja la Israel limeripoti kuwa Netanyahu anapania kumpa Trump taarifa za kiintelijensia kuhusu mpango wa makombora wa Iran, pamoja na mauaji ambayo Iran imeyafanya dhidi ya raia wake, wakati wa maandamano ya wiki chache zilizopita ya kuipinga serikali.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW