SiasaMarekani
Netanyahu na Zelensky ziarani Marekani
28 Julai 2026
Matangazo
Viongozi hao watatumia pia fursa hiyo kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump. Graham aliyefariki Julai 11 akiwa na umri wa miaka 71, alikuwa mmoja wa washirika na watetezi wakubwa wa Israel na Ukraine huko Washington. Huu utakuwa mkutano wa kwanza kati ya Trump na Netanyahu tangu kuanza kwa vita vya Iran, mada ambayo itagubika mazungumzo yao. Itakumbukwa kuwa katika miezi ya karibuni, Trump na Netanyahu walitofautiana kuhusu namna ya kuumaliza mzozo huo.
Hata hivyo Trump na Zelensky wamekutana mara kadhaa lakini rais huyo wa Ukraine amekuwa na wasiwasi kutokana na White House kuonekana kuitupilia Kyiv na kuelekeza nguvu zote katika mzozo wa Mashariki ya Kati.