1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK: Mrithi wa Annan ajulikane ifikapo Oktoba

28 Septemba 2006

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekubali kuwa mrithi wa Katibu Mkuu Kofi Annan,lazima achaguliwe hadi mwisho wa mwezi Oktoba.Kati ya wagombea 7,alieshika nafasi ya mbele katika chaguzi mbili zisizo rasmi katika Baraza hilo lenye wanachama 15,ni waziri wa mambo ya kigeni wa Korea ya Kusini,Ban Ki-Moon.Yeye ameapa kupunguza urasimu na kufanya mabadiliko yatakayosaidia kazi kufanywa kwa mafanikio zaidi. Mwezi wa Desemba,Kofi Annan anakamilisha miaka yake kumi kama Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW