1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK: UN kuafikiana na US juu ya Iraq

20 Januari 2004

Umoja wa Mataifa umeanza kutafakari pendekezo la Marekani na serikali ya mpito ya Iraq ya kumuomba Katibu Mkuu Kofi ANNAN atume wajumbe wake kwenda Baghdad kuangalia iwapo mazingira yaliopo yanatoa fursa ya kufanyika uchaguzi kabla ya mwisho wa mwaka huu. Matokeo ya ziara hiyo yanatarajiwa kusaidia kuondoa tafauti kati ya Marekani na kiongozi mkuu wa Washi'a wa Iraq kuhusu masharti ya Marekani kuwakabidhi Wairaki madaraka ifikapo Juni 30 kama ilivyotakiwa na Umoja wa Mataifa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW