1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK: Watu milioni 2.5 wakabiliwa na njaa nchini Niger

20 Julai 2005

Umoja wa mataifa umesema kwamba Niger inakabiliwa na tatizo kubwa la kibinadamu. Maofisa wa umoja huo na madaktari walio katika taifa hilo la Afrika magharibi wanasema watoto wanafariki dunia kwa sababu ya njaa kwa kuwa ulimwengu umepuuza miito ya kupeleka misaada ya chakula nchini humo.

Mazao ya chakula yalikuwa mabaya mno kufuatia ukame na mimea kuharibiwa na wadudu. Watu milioni 2.5 wanahitaji kwa dharura chakula wakiwemo watoto elfu 800.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW