NEW YORK:Waandishi wa Marekani waachiwa huru Ethiopea
23 Mei 2007Matangazo
Waandishi wa habari watatu wa gazeti la New York Times waliyokuwa wakishikiliwa na majeshi ya Ethiopea kwa muda wa siku tano wameachiwa.
Gazeti hilo limesema kuwa waandishi hao akiwemo mkuu wa kituo cha Nairobi, walikamatwa tarehe 16 mwezi huu katika jimbo la Ogaden nchini Ethiopea karibu na mpaka na Somalia.
Limesema kuwa waandishi hao ambao walikuwa kikazi katika eneo hilo walinyanyaswa ikiwa ni pamoja na kupigwa wakati walipokamatwa, ambapo hawakuelezwa sababu ya kukamatwa kwao.