1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ngao ya Jamii: Yanga ama Simba?

Saumu Njama Mhindi Joseph
15 Septemba 2025

Pazia la Ligi kuu soka Tanzania Bara linafunguliwa wiki hii huku Jumanne septemba 16 Wadau wa soka wanasubiri kwa hamu pambano la kukata na shoka litakalowakutanisha watani wa jadi Simba na Yanga.

Kandanda- Tanzania
Mashabiki wa Simba wasema mechi dhidi ya Yanga ni ngumu kubashiri lakini wanaimani na kikosi msimu huu.Picha: BackpagePix/empics/picture alliance

Historia haitoshi kuamua nani atashinda  Pambano hilo la Ngao ya Jamii kwani kila mechi ya Ngao ya Jamii huleta ushindani wa hali ya juu, na mara nyingi mafanikio hutoka kwa maandalizi, morali ya timu, na mikakati ya kocha.

Kocha wa Simba Fadlu Davis ametoa kauli hii kuelekea mchezo huo.

"Tumekuwa na maandalizi mazuri kabla ya msimu na tuko tayari Bila shaka, kuna wachezaji wengi wapya, pamoja na wachezaji wa msingi ambao wamebaki Kwa hivyo tuko na hamu kubwa kuona msimu unapoanza na nani anaweza kucheza Derby Tuna hamu kubwa kwa mchezo huu na ni mtihani mkubwa kwetu Sio kwetu tu bali pia kwa wachezaji wadogo Mabingwa wawili wakubwa wakikabiliana uso kwa uso tunaweza hkutegemea mchezo wa kusisimua"Amesema Kocha wa Simba Kocha wa Simba Fadlu Davis

Beki wa Simba Shomari kapombe amesema wachezaji wamejiandaa vizuri kuelekea mchezo huo.

"Tmefanya maandalizi Vizuri na tumepokea mafunzo mengi kutoka katika benchi letu la ufundi utakuwa ni wakati mzuri kuelekea katika mchezo huu na sisi kama wachezaji tupo Tayari "Amesema Beki wa Simba Shomari kapombe.

Ushindani utakuaje?

Mashabi wa Yanga wasema mechi itakuwa ngumu kwa sababu timu zote zimejipanga.Picha: DW/E. Boniphace

Kwa upande wa Yanga kocha Romain Folz anabainisha kuwa mechi hiyo itakuwa ya ushindani.

"Tuna wachezaji wengi ambao wanaweza kucheza katika nafasi hiyo Naweza kukuhakikishia kwamba yeyote nitakayemchagua kuanza au kuingia kwenye mchezo kesho atafanya vizuri Atatoa kiwango kizuri Iwe ni Balla cont'e , iwe ni Aziz, hata Duke anaweza kucheza katika nafasi hiyo Tuna wachezaji wengi ambao wanaweza kucheza pale Wote wana uwezo wa kutoa kiwango kizuri Kwa hivyo kwangu mimi"Amesema Kocha mkuu wa yanaga Romain Folz

Beki wa Yanga SC, Dickson Job amesema ni wajibu wa wachezaji kupambana ili kupata matokeo.

"kwa niaba ya wachezaji sisi kama wachezaji tupo tayari kwa ajili ya mchezo huo kwani tunaamini utakuwa mchezo mgumu lakini sisi kama wachezaji ni wajibu wetu kwenda kupambana kupata matokeo"Amesema Beki wa Yanga SC, Dickson Job

Mashabiki wa Simba na Yanga wamezungumzia kuelekea mchezo huo.

"Mechi ya kesho ya Ngao ya Jamii inaenda kwa upande wetu simba sports klabu tunaenda kulipa kisasi hatuwezi kukaa kinyonge kwa muda mrefu ''Amesema shabiki wa Simba Augstino Madehe

"Kwa upande wangu mimi kama shabiki wa Yanga naiona ni mechi ambayo itakuwa ni tafu kwa sababu Timu zote zimejipanga ni mechi itakuwa ngumu kwa uwanjani"Amesema shabiki wa Yanga Mussa Nangale

Pambano hilo muhimu litachezwa saa 11 jioni kwa saa za Tanznaia katika uwanja wa Benjamin Mkapa kuashiria ufunguzi wa msimu  wa ligi kuu soka Tanzania Bara katika msimu wa 2025/26.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW