Sheria na HakiAmerika ya Kaskazini
Nicolas Maduro afikishwa mahakani nchini Marekani
5 Januari 2026
Matangazo
Maduro anafikishwa mahakamani siku mbili baada ya kukamatwa katika operesheni ya kijeshi ya Marekani pamoja na mkewe Cilia Flores.
Maduro anadaiwa kutumia mamlaka yake ambayo Marekani inayaona kuwa yalipatikana kinyume cha sheria kuwezesha maelfu ya tani za kokeini kuingizwa nchini Marekani ili kujinufaisha.
Aidha madai yaliyochapishwa na Mwanasheria Mkuu wa Marekani Pam Bondi kwenye mtandao wa X, yanaonyesha kuwa Maduro pia alikuwa akishirikiana na wafanyabiashara wa dawa hizo.
Maduro aliwahi kushitakiwa nchini Marekani kwa madai kama hayo mwaka 2020, ikimaanisha kimsingi anakabiliwa na mashtaka yaliyorekebishwa na siyo mapya kabisa.