1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nielsen atafuta suluhu la kidiplomasia kwa Greenland

15 Januari 2026

Waziri mkuu wa Greenland Jens-Frederik Nielsen, ametoa wito leo wa mazungumzo ya kutatua mvutano kuhusu kisiwa hicho kinachojitawala, siku moja baada ya kufanyika kwa mazungumzo juu ya mustakabali wa eneo hilo.

Jens-Frederik Nielsen
Waziri mkuu wa Greenland, Jens-Frederik NielsenPicha: Johan Nilsson/TT/Kod 50090/picture alliance

Katika chapisho kwenye mtandao wa Facebook, Nielsen amesema mazungumzo na diplomasia ndio njia sahihi hata katika wakati ambapo shinikizo ni kubwa.

Alipongeza ukweli kwamba mazungumzo sasa "yanaendelea" kufuatia mkutano wa ngazi ya juu katika Ikulu ya White House ambao umeshindwa kutatua tofauti juu ya suala hilo.

Wakati huo huo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Urusi amesema wanakubaliana na China kwamba haikubaliki kuendelea kudaiwa kwamba nchi hizo zinapanga njama kuhusu Greenland.

Haya yanajiri huku Uholanzi ikisema leo kuwa itampeleka afisa mmoja wa kijeshi kuunga mkono ujumbe wa Ulaya huko Greenland katika wakati ambapo Trump ameapa kuchukuwa udhibiti wa eneo hilo .

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW