1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nigeria yaweka marufuku ya kutembea kuzuwia uporaji chakula

31 Julai 2023

Mamlaka za jimbo la Adamawa kaskazini mashariki mwa Nigeria imeweka marufuku ya masaa 24 ya kutembea nje ili kuzuwia uporaji wa maghala ya chakula katika mji mkuu wa jimbo hilo wa Yola.

Karte Nigeria Überschwemmung Niger und Benue EN

Uporaji huo ulishuhudia mamia ya wakaazi wakivunja maghala ya umma na binafsi yanayohifadhi nafaka na bidhaa nyingine na kuondoka navyo. 

Msemaji wa polisi ya Adamawa, Yahaya Nguroje, alisema maafisa usalama wamepelekwa ili kusimamia utekelezaji wa amri hiyo iliyotangazwa na gavana wa jimbo hilo, Ahmadu Umaru Fintiri, kupitia taarifa iliyosomwa na msemaji wake, Humwashi Wonosikou. 

Soma zaidi: Boko Haram wapanga kuzishambulia balozi za Marekani, Uingereza

Mwezi uliyopita, Nigeria ambayo ndiyo nchi yenye wakazi wengine zaidi barani Afrika na taifa lenye uchumi mkubwa zaidi, ilisitisha mpango wa ruzuku ya mafuta, na kusababisha bei za petroli kupanda mara nne na kuongezeka kwa bei za vyakula.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW