1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ntanganda yuko korokoroni ICC

23 Machi 2013

Mtuhumiwa wa uhalifu wa kivita Bosco Ntaganda, ambaye anajulikana kwa jina la utani la "The Terminator",amewekwa korokoroni katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu leo Jumamosi(23.03.2013),mjini The Hague.

Fugitive Congolese warlord Bosco Ntaganda attends rebel commander Sultani Makenga's wedding in Goma December 27, 2009. Ntaganda walked into the U.S. Embassy in Rwanda on March 18, 2013 and asked to be transferred to the International Criminal Court, where he faces war crimes charges racked up during years of rebellion. Picture taken December 27, 2009. REUTERS/Paul Harera (DEMOCRATIC REPUBLIC OF CONGO - Tags: CIVIL UNREST CRIME LAW MILITARY POLITICS SOCIETY)
Bosco NtagandaPicha: Reuters

Ntaganda amejisalimisha mwenyewe ili kuruhusu akabiliane na madai ambayo ni pamoja na mauaji, ubakaji na kuwatumia watoto kama wanajeshi.

Mtuhumiwa wa kwanza kuweza kujisalimisha binafsi kwa mahakama hiyo ya ICC, Ntaganda anatakiwa kwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu, madai ambayo anadaiwa yalifanyika wakati akiwa mbabe wa kivita katika eneo la mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Ajisalimisha katika ubalozi wa Marekani

Aliingia katika ubalozi wa Marekani nchini Rwanda siku ya Jumatatu na aliomba apelekwe katika mahakama hiyo mjini The Hague.

Ntaganda anadai kuwa alihusika katika mauaji ya kinyama ya kiasi ya watu 800 katika vijiji katika eneo lenye matatizo la mashariki ya Kongo. Pia anatuhumiwa kuwatumia watoto kama wanajeshi katika jeshi lake la waasi na kuwaweka wanawake kama watumwa wa ngono kati ya Septemba mwaka 2002 na Septemba mwaka 2003.

Alipelekwa katika mahabusu ya ICC mjini Kigali na kusafirishwa hadi katika uwanja wa ndege wa mjini Rotterdam. Mahakama ya ICC ilisema katika ukurasa wake wa Tweeter baada ya Bosco Ntaganda aliwasili katika kituo cha kuwahifadhi watuhumiwa cha ICC, akiwa chini ya ulinzi wa polisi wa Uholanzi katika kitongoji cha mji wa The Hague cha Scheveningen.

Fatou BensoudaPicha: AFP/Getty Images

Ntaganda, ambaye amezaliwa mwaka 1973, atakuwa Mwafrika wa tano kuingia katika mahabusu ya ICC. Atakabiliana na majaji kwa mara ya kwanza siku ya Jumanne, baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kiafya.

Majaji watathibitisha utambulisho wake na lugha ambayo ataweza kufanya mawasiliano ili kuweza kuelewa yale yanayozungumzwa mahakamani na pia atafahamishwa mashtaka dhidi yake, mahakama hiyo imesema.

Bensuda afurahishwa

Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC, Fatou Bensouda amekaribisha taarifa hizo za kusafirishwa kwa Ntanganda, akisema kuwa "Hii ni siku nzuri sana kwa wahanga katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na pia kwa sheria za kimataifa. Leo wale ambao wanadaiwa kuwa waliteseka kutokana na Bosco Ntaganda wanaweza kuwa na matumaini juu ya uwezekano wa sheria kuchukua mkondo wake," amesema katika taarifa.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani, John Kerry amesifu kuwa hiyo ni hatua kubwa iliyopigwa, "kwa sheria na uwajibikaji." "Sasa yapo matumaini kuwa haki itatendeka," amesema katika taarifa.

John KerryPicha: Reuters

Kuwasili kwa Ntaganda mjini The Hague "pia kutatoa ishara nzito kwa wale wote wanaotenda vitendo vya kinyama kuwa watawajibishwa kwa uhalifu wao," Kerry amesema.

Geraldine Mattioli-Zeltner wa shirika la Human Rights Watch , amesema kuwa kuwasili kwa Ntaganda katika mahakama ya ICC " kutakuwa ushindi mkubwa kwa wahanga wa mauaji mashariki mwa Kongo na wanaharakati wa eneo hilo ambao wamefanya kazi katika hali ya tahadhari kubwa kwa ajili ya kukamatwa kwake.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe

Mhariri: Grace Patricia Kabogo

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW