Nusu ya raia Sudan Kusini wanakabiliwa na njaa kali
26 Novemba 2025
Matangazo
Watu wa Sudan Kusini wanakabiliwa pia na na huduma duni ya maji safi. Idadi ya watu wanaokabiliwa na njaa kali inatarajiwa kupanda hadi kufikia milioni 7.5 ifikapo mwezi Aprili mwakani.
Mataifa wafadhili yamepunguza bajeti ya misaada
Oxfam imesema hadi sasa ni asilimia 40 pekee ya dola bilioni 1.6 za mpango wa msaada kwa taifa hilo changa zaidi barani Afrika ndiyo ambayo imeshatolewa. Upungufu huo unatokana na mataifa ya Magharibi kupunguza bajeti zao za misaada.
Sudan Kusini ilikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa kipindi cha miaka mitano hali iliyosababisha zaidi ya raia milioni 2 kuyahama makazi yao. Nchi hiyo licha ya hali ngumu inawahifadhi maelfu ya wakimbizi kutoka taifa jirani la Sudan lialokabiliwa na vita.