SiasaMarekani ya Kusini
120 wauawa Brazil katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya
30 Oktoba 2025
Matangazo
Miili ya waliouawa imeshuhudiwa ikiwa imepangwa katika mtaa mmoja usiku wa kuamkia Alhamisi. Taarifa ya polisi imesema mapambano hayo yalilenga kuwafurusha watuhumiwa kuelekea eneo la msitu ambako kikosi maalumu kilikuwa kikisubiri kuwafanyia shambulio la kushtukiza.
Vifo zaidi vinatarajiwa kuongezeka
Idadi ya waliouawa katika purukushani hizo inatarajiwa kuongezeka kwa mujibu wa mamlaka za Rio de Janeiro, Mkuu wa usalama wa mji huo ameahidi kufanya uchunguzi ili kubaini kama polisi walifanya ukiukaji wa aina yoyote wakati wa zoezi hilo.