1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Operesheni kuu Irak dhidi ya al-Qaeda

26 Januari 2008

BAGHDAD:

Waziri Mkuu wa Irak,Nuri al-Maliki amesema,majeshi yake yameanzisha operesheni muhimu dhidi ya wanamgambo wa al-Qaeda.Alipozungumza mjini Karbala,al-Maliki alisema,vikosi vya Irak vimepelekwa mji wa Mosul ulio kaskazini mwa nchi kuteketeza ngome kuu ya mwisho ya waasi wa Kisunni.

Serikali ya Irak inawalaumu wapiganaji wa al-Qaeda kwa mripuko mkubwa uliotokea mjini Mosul siku ya Jumatano na kuua hadi watu 35.Shambulizi hilo pia liliwajeruhi kama watu 200 wengine.

Maafisa wa majeshi ya Marekani wanasema,magaidi wa al-Qaeda wamejikusanya upya katika mikoa ya kaskazini baada kufukuzwa kwa nguvu kutoka wilaya ya magharibi ya Anbar na mjini Baghdad.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW