1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hungary yaionya LGBTQ dhidi ya kuadhimisha siku yao

27 Juni 2025

Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban amesema polisi hawatoyasambaratisha maadhimisho ya kila mwaka ya kundi la watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja LGBTQ, yanayotarajiwa kufanyika jumamosi (28.06.2025).

Hungary |Viktor Orbán
Waziri Mkuu wa Hungary Viktor OrbánPicha: Omar Havana/AP/picture alliance

Maadhimisho haya yanayofanyika katika mji mkuu wa taifa hilo Budapest, licha ya Orban kulipiga marufuku kundi hilo.

Orbnan lakini ametoa onyo kwa waandaaji na washiriki kuhusu matokeo ya kisheria.  

Serikali ya muungano inayoogozwa na Orban mapema mwaka huu ilifanyia mabadiliko sheria na katiba ya nchi, kuyapiga marufuku maadhimisho hayo ya kila mwaka, akidai kuwalinda watoto. 

Marekani yawaonya raia wake walio ugenini kuhusu uwezekano wa matukio ya LGBTQ kushambuliwa

Wiki iliyopita polisi iliyazuwia maadhimisho hayo ikisema watakaoshiriki watakabiliwa na mkono wa sheria ikidai hatua yake inazuwia kueneza taarifa za LGBTQ kwa watoto walio chini ya miaka 18.

Hata hivyo wandaaji na washiriki wameendelea kusisitiza kuwa mipango yao itaendelea licha ya onyo hilo.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW