Ouattara ahutubia taifa
8 Aprili 2011Akizungumza jana usiku kupitia televisheni ya nchi hiyo, Ouattara ameyatolea wito pia majeshi yake kudumisha utaratibu katika mji mkuu wa nchi hiyo Abidjan, ambako wanamgambo wanaorandaranda katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya wizi na kufanya mashambulio yasiyo na mpangilio maalumu.
Katika hatua nyingine katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa ban Ki Moon amemtaka Rais Gbagbo kuachia madaraka mapema kabla ya kuchelewa.
Amesema hiyo ni fursa ya mwisho kwa gbagbo kuondoka vizuri katika nafasi hiyo na kumkabidhi madaraka Ouattara.
Wakati huohuo, ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Cote d'Ivoire umesema utamkamata gbagbo akiwa hai na kumfungulia mashtaka.
Ouattara amekuwa akisisitiza juu ya Gbagbo kukamatwa akiwa hai, licha ya kwamba majeshi yake yamekuwa yakitoa upinzani mkali.