SiasaSaudi Arabia
Pakistan, Saudi Arabia zasaini ushirikiano wa ulinzi
18 Septemba 2025
Matangazo
Makubaliano haya muhimu yamefikiwa kufuatia shambulio la Israel dhidi ya Qatar wiki iliyopita. Ufalme wa Saudi Arabia kwa muda mrefu umekuwa na uhusiano wa karibu wa kiuchumi, kidini na kiusalama na Pakistan, ikiwa ni pamoja na kuripotiwa kufadhili mpango wa silaha za nyuklia wa Islamabad wakati ulipokuwa ukitengenezwa.
Hata hivyo, muda wa kusainiwa kwa mkataba huu unaonekana kuwa ujumbe kwa Israel, ambayo kwa muda mrefu imeshukiwa kuwa taifa pekee la Mashariki ya Kati lenye silaha za nyuklia, na ambalo limeendesha mashambulizi makubwa ya kijeshi tangu shambulio la Hamas dhidi ya Israel tarehe 7 Oktoba 2023, likizihusisha Iran, Lebanon, Mamlaka ya Palestina, Qatar, Syria na Yemen.