1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroPakistan

Pakistan yasema imeshambulia vituo vya kijeshi Afghanistan

Saleh Mwanamilongo
15 Machi 2026

Kumekuwa na mapigano ya mara kwa mara mpakani katika wiki za hivi karibuni, yakikwamisha biashara na kulazimu wakazi wa maeneo ya karibu kuyahama makazi yao.

Afghanistan Daman 2026 | Moshi wafuka baada ya mashambulizi ya anga ya Pakistan kwenye maghala ya mafuta karibu na Kandahar
Islamabad ilizindua operesheni ya kijeshi dhidi ya Afghanistan mwezi uliopita, ikilenga kile ilichokiita wanamgambo wa Kiislamu kufuatia mashambulizi nchini PakistanPicha: AFP

Mvutano wa kijeshi unaendelea kati ya Pakistan na Afghanistan baada ya Islamabad kusema kuwa jeshi lake limefanya mashambulizi dhidi ya vituo vya kijeshi na maficho ya wanamgambo kusini mwa Afghanistan.

Kwa mujibu wa vyanzo vya usalama, mashambulizi hayo yalilenga miundombinu ya kijeshi na ghala la vifaa katika mji wa Kandahar, ambao pia ni ngome ya kiongozi mkuu wa Taliban, Hibatullah Akhundzada. Shambulio lingine liliripotiwa kulenga handaki linalodaiwa kutumiwa na wapiganaji wa Taliban na kundi la TTP.

Wakaazi wa Kandahar wamesema waliona ndege za kijeshi angani na kusikia milipuko usiku. Serikali ya Taliban kupitia msemaji wake Zabihullah Mujahid imesema mashambulizi hayo yalisababisha uharibifu mdogo katika kituo cha kuwasaidia waraibu wa dawa.

Mapigano katika mpaka wa nchi hizo yameongezeka katika wiki za hivi karibuni, huku Umoja wa Mataifa ukisema takribani raia 75 wameuawa na zaidi ya 190 kujeruhiwa tangu mwishoni mwa Februari.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW