1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa ajaye atakabiliana na hoja ngumu

7 Mei 2025

Mkuu wa Chuo cha Makadinali wa Kanisa Katoliki amewahimiza viongozi wenzake wa kidini kuchagua Papa ajaye, atakayekuwa na uwezo wa kutoa mwongozo katika "mabadiliko magumu katika nyakati ngumu za kihistoria."

Vatikan 2025 | Kardinäle bei Messe zur Papstwahl vor Beginn des Konklaves
Picha: Us Vatican Media/IMAGO/ZUMA Press/IMAGO

Katika misa ya mwisho kabla ya kufunguliwa kwa kongamano la kupiga kura, Kadinali Giovanni Battista Re pia alitoa wito kwa makadinali hao watakaopiga kura kudumisha umoja wa Kanisa, akisema ni uamuzi wa muhimu wa kipekee, na kila fikira za kibinafsi lazima ziwekwe kando.

Soma pia: Merkel: Ni vyema Papa ajaye akafuata mkondo wa Papa Francis

Waumini wa Kanisa Katoliki na wafuatiliaji wengine kote duniani watasubiri ishara ya kuchaguliwa kwa papa mpya kupitia moshi utakaotoka kwenye chimni iliyofungwa juu ya Kanisa la Sistine.

Moshi mweupe utakapofuka itakuwa ni ishara kuwa baraza hilo la makadinali limefanikiwa kumchagua kiongozi mpya wa kanisa Katoliki.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW