1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa awataka maaskofu kuzungumzia sera za uhamiaji za Trump

8 Oktoba 2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo XIV amewataka maaskofu wa Marekani kuzungumzia sera kali za Rais Donald Trump kwa wahamiaji.

Vatikan Rom 2025 | Privataudienz von Papst Leo XIV. mit Bundespräsident Frank-Walter Steinmeier
Picha: Vatican Media/ZUMA/dpa/picture alliance

Papa ameyasema haya wakati akizungumza na maaskofu hao waliokuwa wamemtembelea huko Vatican Jumatano.

Hili ni shinikizo la hivi karibuni la kiongozi huyo wa kidini katika suala hilo.

Wakati wa mkutano na maaskofu hao na wafanyakazi wa kijamii kutoka mpaka wa Mexico na Marekani, Papa Leo ambaye ndiye kiongozi wa kwanza wa Kanisa Katoliki kutoka Marekani, alikabidhiwa dazeni kadhaa za barua kutoka kwa wahamiaji zinazoelezea hofu yao ya kurudishwa makwao chini ya sera za utawala wa Trump.

Ikulu ya Marekani, White House inasema Trump alichaguliwa kutokana na ahadi zake nyingi alizotoa ikiwemo kuwarudisha makwao wahamiaji haramu. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW