1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa Francis kutangaza makadinali wapya 21

Sylvia Mwehozi
9 Julai 2023

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amesema kwamba atatangaza Makadinali wapya 21 kutoka maeneo tofauti ya ulimwengu mwishoni mwa mwezi Septemba.

Papa Francis
Papa Francis, kiongozi wa Kanisa Katoliki dunianiPicha: Stefano Spaziani/picture alliance

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amesema hii leo kwamba atatangaza Makadinali wapya 21 kutoka maeneo tofauti ya ulimwengu mwishoni mwa mwezi Septemba. Baraza hilo la Makadinali ni la tisa kuundwa chini ya Papa Francis ambaye utawala wake umefikisha miaka 10.

Uteuzi wa Makadinali wapya utakuwa ukitizamwa kwa ukaribu kama ishara ya mwelekeo wa baadaye wa Kanisa Katoliki na vipaumbele vyake kwa waumini wake wapatao bilioni 1.3.

Makadinali walio chini ya umri wa miaka 80 watashiriki katika zoezi la kumteua mrithi wa Francis. Tangu alipokuwa Papa, Francis amejaribu kuwapandisha madaraja makasisi kutoka mataifa yanayoendelea mbali na Roma kama sehemu ya falsafa yake ya ujumuishwaji.Mjadala Vatican juu ya mageuzi ndani ya kanisa Katoliki

Makadinali watakaotangazwa mwishoni mwa Septemba ni kutoka katika maeneo ambayo Ukristo unazidi kukua ikiwemo Afrika, Amerika ya Kusini na Asia.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW