Papa Leo kutoa baraka maalum za Pasaka huko Vatican
5 Aprili 2026
Matangazo
Leo, papa wa kwanza mzaliwa wa Marekani, amehutubia waumini katika Uwanja wa Mtakatifu Petro huko Vatican uliopambwa kwa mawaridi meupe ambapo maelfu ya waumini walikusanyika .
Papa Leo aliwasihi waumini kudumisha matumaini mbele ya vifo, vinayonyemelea kupitia udhalimu, ubinafsi wa kibaguzi, katika ukandamizaji wa maskini na kutowajali wanyonge.
Baadaye atatoa ujumbe maalumu wa kitamaduni kwa wakazi wa Roma na duniani nzima unaojulikana kama Urbi et Orbi.
Kulingana na mafundisho ya Biblia, Pasaka husherehekewa kuadhimisha ufufuko wa Yesu Kristo.