Papa Leo: Vita vya Mashariki ya kati ni janga la kibinaadamu
22 Machi 2026
Kiongozi huyo wa kidini ameyasema hayo huku akiendeleza wito wake wa kutaka vita hivyo visitishwe mara moja.
Wakati vita vya Israel na Marekani dhidi ya Iran vikiingia wiki yake ya nne , Papa huyo wa kwanza kutoka Marekani, amesema anafuatilia kwa hofu kubwa hali ya Mashariki ya kati na maeneo mengine yanayokumbwa na vita.
"Ninaendelea kufuatilia kwa masikitiko makubwa hali ilivyo Mashariki ya Kati, na pia katika maeneo mengine ya dunia yanayokumbwa na vurugu. Hatuwezi kukaa kimya wakati watu wengi wasiokuwa na hatia, ambao ni waathirika wa vita hivi wakiumia. Kinachowaumiza kinawaumiza wanadamu wote. Vifo na mateso vinavyosababishwa na vita hivi ni janga kwa dunia nzima na hata mbele za Mungu."
Akizungumza katika uwanja wa Kanisa la Mtakatifu Peter, Papa Leo, amesema ni muhimu kuomba ili kukemea uchokozi na ukatili unaoendelea duniani ili kufungua njia ya uwepo wa amani.