1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maelfu ya raia kushiriki misa na Papa Leo XIV mjini Douala

17 Aprili 2026

Maelfu ya watu wamekusanyika mjini Douala nchini Cameroon katika misa kubwa itakayoongozwa na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo XIV. Ibada hiyo inatajwa kuwa tukio kubwa zaidi katika ziara yake barani Afrika.

Papa Leo XIV katika Kanisa la Mtakatifu Joseph mjini Bamenda, Cameroon
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo XIVPicha: Guglielmo Mangiapane/REUTERS

Tukio hilo limewakusanya karibu watu laki sita kwenye mitaa inayouzunguka uwanja wa Japoma watakaposikiliza hotuba ya Papa. Idadi kubwa ya watu wenye shauku ya kumsikia na kumuona kiongozi huyo waliingia katika viwanja hivyo tangu jana kwa ajili ya tukio hilo.

Papa Leo na ujumbe wa amani kwa Afrika

Awali siku ya Alhamisi, Papa Leo XIV alitoa ujumbe mzito mjini Bamenda kulikoathiriwa na vita ambako alitoa wito wa mabadiliko na kuithamini amani. Papa Leo amewakosoa pia wageni wanaoinyonya Afrika na kuongeza kuwa wanachangia umasikini na ukosefu wa maendeleo barani humo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW