1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Pezeshkian asema Iran itajikwamua dhidi ya vikwazo vyovyote

20 Septemba 2025

Rais wa Iran Masoud Pezeshkian ameapa leo kwamba nchi yake itajikwamua dhidi ya vikwazo vyovyote vipya, hiyo ni baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupiga kura ya kutoondoa kabisa vikwazo dhidi ya nchi hiyo.

Iran Tehran 2025 | Rais Masoud Pezeshkian
Rais wa Iran Masoud PezeshkianPicha: Iranian Presidency/ZUMA/picture alliance

Katika matamshi yaliopeperushwa na shirika la habari la serikali, Pezeshkian amesema kupitia mchakato huo wa kuiwekea tena Iran vikwazo, mataifa ya magharibi yanafunga barabara lakini ni akili na mawazo yanayofungua au kujenga barabara.

Rais huyo pia amesema hawatasalimu amri chini ya shinikizo kwa sababu wana uwezo wa kubadilisha hali hiyo.

Mchakato huo utaweka tena vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran ikiwa makubaliano kuhusu mpango wa nyuklia ya Iran hayatafikiwa kati ya Tehran na mataifa ya Ulaya yenye nguvu ndani ya wiki moja.