1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi wa Uganda wakanusha madai ya kukamatwa kwa Bobi Wine

17 Januari 2026

Polisi wa Uganda wamekanusha madai yaliyotolewa na chama cha kiongozi wa upinzani Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine.

Uganda Kampala 2026 | Kiongozi wa upinzani Bobi Wine katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu uchaguzi wa rais
Kiongozi wa upinzani Bobi Wine katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu uchaguzi wa raisPicha: Rian Cope/AFP/Getty Images

Polisi wa Uganda wamekanusha madai yaliyotolewa na chama cha kiongozi wa upinzani Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine, kwamba kiongozi huyo alikamatwa na wanajeshi wakati Rais Yoweri Museveni akielekea kupata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa wiki hii.

Chama cha Bobi Wine cha National Unity Platform (NUP) kilitoa taarifa jana usiku kwamba helikopta ya jeshi ilitua katika makazi yake huko Kampala na kumchukua kwa nguvu na kumpeleka sehemu isiyojulikana. Hata hivyo msemaji wa polisi wa kitaifa, Kituuma Rusoke, amedai kuwa Wine yupo nyumbani kwake na yuko huru kusafiri.

Hadi kufikia leo asubuhi, Museveni ambaye ameiongoza Uganda tangu mwaka 1986 alikuwa akiongoza kwa karibu 72% ya kura, kwa mujibu wa tume ya uchaguzi. Wine anafuatia akiwa na 24%, huku zaidi ya asilimia 90 ya vituo vya kupigia kura vikiwa tayari vimehesabiwa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW