1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi yakabiliana na waandamanaji mjini Essen Ujerumani

29 Juni 2024

Waandamanaji na polisi wamekabiliana asubuhi ya leo katika mji wa magharibi wa Ujerumani wa Essen, katika eneo ambalo kunafanyika kongamano la siku mbili la chama cha mrengo wa kulia Alternative for Germany AfD.

Ujerumani | Mkutano wa chama cha AfD huko Essen |Mapigano kati ya waandamanaji na polisi
Waandamanaji wakiwa wamekaa mbele ya polisi kwenye barabara ya kuingilia kwenye eneo la mkutano wa chama cha AFD.Picha: Henning Kaiser/dpa/picture alliance

Msemaji wa polisi amesema kundi kubwa la waandamanaji lilifanya jaribio la kuvunja vizuizi vya polisi hatua ambayo jeshi hilo lililazimika kuwapulizia maji ya kuwasha na kutumia fimbo ili kuwadhibiti wasiendelee.

Hata hivyo haikuweza kufahamika mara moja kama kuna waliojeruhiwa. Katika mji huo wa Essen kunatarajiwa kufanyika maandamano ya hadi watu 100,000 leo hii. Mamlaka imekuwa na wasiwasi kwamba, wakati maandamano jumla yakitarajiwa kuwa ya amani, karibu watu 1,000 wenye itikadi kali za mrengo wa kushoto wangetumia njia za vurugu kuvuruga mkutano.

Takriban wajumbe 600 wa chama cha AfD wanakutana katika mji huo na viongozi wenza wa sasa Alice Weidel na Tino Chrupalla ambao wanataka kuchaguliwa tena kabla ya uchaguzi wa wabunge wa Ujerumani katika msimu wa mapukutiko mwaka ujao.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW