PORT HARCOURT: Mateka sita raia wa Urusi waachiwa huru
8 Agosti 2007Matangazo
Raia sita wa Urusi waliotekwa nyara zaidi ya miezi miwili kusini mwa Nigeria katika jimbo lenye utajiri wa mafuta na Niger Delta wamechiwa huru.
Raia hao wa Urusi wanaume wanne na wanawake wawili walitekwa nyara mwanzoni mwa mwezi Juni.
Hakuna taarifa zaidi zilizotolewa kuhusiana na kuachiliwa kwao.