Pumzika kwa amani Diogo Jota
5 Julai 2025
Ibada ya mazishi ilifanyika katika kanisa la Igreja Matriz katika mji wa Gondomar, Ureno, ambako Jota alikuwa na makazi.
Kocha wa timu ya taifa ya Ureno, Roberto Martínez, pamoja na wachezaji kadhaa maarufu wa Ureno walihudhuria, wakiwemo Bernardo Silva na Rúben Dias wa Manchester City, na Bruno Fernandes wa Manchester United.
Wazazi wa marehemu walihudhuria ibada hiyo katika Kanisa la São Cosme, karibu na Porto, pamoja na Rais wa Ureno Marcelo Rebelo de Sousa, Waziri Mkuu Luís Montenegro, na wakala wa Jota.
Jota, mwenye umri wa miaka 28, na kaka yake André Silva, 25, walikutwa wamefariki karibu na mji wa Zamora, kaskazini-magharibi mwa Uhispania, mapema Alhamisi baada ya gari lao aina ya Lamborghini kupata ajali na kuwaka moto usiku wa manane.