Putin: Naamini Urusi itashinda vita vyake dhidi ya Ukraine
31 Desemba 2025
Matangazo
Putin amewapongeza wapiganaji na makamanda akisema anawaamini na anaamini taifa hilo litashinda vita hivyo.
Wanajeshi wake ambao Ukraine imewashutumu kutekeleza uhalifu wa kivita wamesifiwa na Putin aliyewaita mashujaa.
Putin ameyasema hayo wakati kukiwa na wasiwasi wa kutanuka kwa mgogoro huo baada ya Urusi kudai Ukraine imeshambulia makaazi ya Putin kwa droni hatua iliyoiita ya kigaidi na inayochochea kudhoofisha juhudi zinazoendelea za amani.
Licha ya hayo Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, alisema atakutana na washirika wake Januari 6 nchini Ufaransa katika juhudi za kuendeleza juhudi za kusaka amani.