1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin azishutumu Ukraine, Magharibi kuchochea mauaji Urusi

27 Juni 2023

Rais Vladimir Putin wa Urusi ameishutumu Ukraine na washirika wake wa nchi za Magharibi kwa kutaka mauaji ya wenyewe kwa wenyewe nchini mwake wakati wa uasi wa mamluki wa kundi la Wagner.

Nach Aufstand der Söldnergruppe Wagner in Russland - Wladimir Putin
Picha: Uncredited/Russian Presidential Press Service/AP/dpa/picture alliance

Katika hotuba yake ya kwanza tangu kulipozuka uasi huo siku ya Jumamosi, Putin alisema alitoa agizo la moja kwa moja la kuepusha umwagikaji mkubwa wa damu na kutoa kinga kwa wapiganaji wa Wagner, ambao uasi wao ulitoa changamoto kubwa zaidi katika utawala wake wa miongo miwili.

Putin alieleza kuwa wapiganaji wa Wagner wanaweza kuchagua kujiunga na jeshi la Urusi, kuelekea Belarus au hata kurudi makwao.

Soma zaidi: Yevgeny Prigozhin aeleza sababu za kufanya uasi

Hapo awali, kiongozi wa kundi la mamluki la Wagner, Yevgeny Prigozhin, naye alivunja ukimya baada ya kutoa tamko kwa mara ya kwanza tangu uasi wa Jumamosi kupitia mkanda wa sauti uliosambazwa kwenye mtandao wa Telegram.

Kiongozi huyo alidai hakuwa na dhamira ya kupindua serikali ya Moscow bali alilazimika kufanya uasi kujibu mashambulizi dhidi ya wapiganaji wake.  

Hadi sasa Prigozhin hafahamiki alipo ingawa alieleza Jumamosi kwamba angelielekea Belarus.  

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW