Qatar yazihimiza Marekani na Iran kuzingatia mazungumzo
13 Aprili 2026
Matangazo
Katika taarifa, wizara ya mambo ya nje ya Qatar imesema wakati wa mazungumzo kwa njia ya simu, Al Thani alitoa wito kwa Araghchi na kusisitiza haja ya kufungua njia za baharini, kuhakikisha uhuru wa safari za meli.
Wakati huo huo, Bahrain imemuita leo balozi wa Iraq nchini humo kuhusu mashambulizi ya droni inayodai yalirushwa kutoka nchini humo kuelekea ufalme huo na mataifa mengine ya Ghuba licha ya usitishaji wa mapigano kati ya Iran na Marekani.
Pia imeitaka nchi hiyo kushughulikia vitisho na mashambulizi hayo haraka iwezekanavyo na kwa uwajibikaji.