1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Raia wa Syria ahukumiwa miaka 13 jela kwa jaribio la mauaji

5 Machi 2026

Mahakama moja mjini Berlin Alhamis imemhukumu kifungo cha miaka 13 jela raia mmoja wa Syria aliyedaiwa kufanya shambulizi la kijihadi kwa kumshambulia kwa kisu mtalii mmoja raia wa Uhispania.

Mshukiwa wa shambulizi la itikadi kali akiwa mahakamani Berlin kabla hukumu kutolewa
Mshukiwa wa shambulizi la itikadi kali akiwa mahakamani Berlin kabla hukumu kutolewaPicha: Sebastian Gollnow/dpa/picture alliance

Shambulizi hilo lilifanyika katika makumbusho ya mauaji ya Holocaust huko mjini Berlin Februari 2025.

Mahakama hiyo imesema mshukiwa huyo mwenye umri wamiaka 20 ambaye ametajwa kwa jina la Wassim tu, amepatikana na hatia ya jaribio la mauaji na uanachama katika shirika la kigaidi.

Shambulizi hilo lililotokea Februari 2025 liliibua hisia kali wakatiambapo kulikuwa na mjadala mkali kuhusiana na uhamiaji, siku chache tu kabla uchaguzi mkuu.

Mshukiwa huyo alikiri kuwa alifanya tukio hilo kutokana na itikadi kali na kwa lengo la kidini.

Ujerumani ina karibu wahamiaji milioni moja kutoka syria, sehemu kubwa ya wahamiaji hao wakiwa waliingia mwaka 2015 wakati wa utawala wa Kansela Angela Merkel.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW