1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Raia wa Venezuela waandamana kuunga mkono upinzani

31 Julai 2024

Maelfu ya raia wa Venezuela waliandamana kwa amani kuunga mkono upinzani siku moja baada ya watu 12 kufariki na wengine kujeruhiwa katika maandamano ya kupinga ushindi wa Rais Nicolas Maduro katika uchaguzi uliomalizika.

Venezuela Caracas | Maandamano
Raia wa Venezuela waandamana kuunga mkono upinzani baada ya uchaguzi tata wa uraisPicha: Jeampier Arguinzones/dpa/picture alliance

Waandamanaji hao mjini Caracas, waliimba wakisema wanataka uhuru huku viongozi wa kisiasa wakisisitiza kwamba walipata kura nyingi za kuhakikishia ushindi.

Miito ya kimataifa imetolewa kwa Baraza la Taifa la Uchaguzi (CNE) linaloegemea upande wa Maduro kutoa maelezo ya kina ya kila hatua kuthibitishia ushindi wa Maduro.

Rais wa Venezuela aamuru jeshi na polisi kushika doria nchi nzima

Maduro amesema upinzani utawajibishwa kwa ghasia za uhalifu, kusababisha majeruhi, vifo na uharibifu unaohusishwa na maandamano hayo.

Shirika la kutetea haki za binadamu la Foro Penal, limesema takriban watu 11, wawili kati yao wakiwa watoto, walifariki katika kile ambacho mkuu wa shirika hilo Alfredo Romero amekielezea kuwa "mgogoro wa haki za binadamu''.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW