1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChina

Rais Trump awasili Beijing kwa mazungumzo na Xi

13 Mei 2026

Rais wa Marekani Donald Trump amewasili Beijing kwa mazungumzo yanayosubiriwa kwa hamu na Rais Xi Jinping wa China yatakayojikita katika mzozo wa nchini Iran, biashara na uamuzi wa Marekani kuiuzia silaha Taiwan.

China Peking 2026 | Donald Trump akishangiliwa baada ya kuwasili uwanja wa ndege
Rais Donald Trump amewasili Beijing China kwa mazungumzo ya ngazi za juu na Rais Xi JinpingPicha: Evan Vucci/REUTERS

Trump alikaribishwa na Makamu wa Rais wa China Han Zheng, pamoja na maafisa wengine waandamizi wa serikali, balozi wa China nchini Marekani na mjumbe wa Washington mjini Beijing, David Perdue.

Mazungumzo muhimu ya mkutano huo wa kilele yatafanyika kesho wakati viongozi hao wawili watakapotembelea eneo ambako watawala wa China walikuwa wakiombea mavuno na ambako kulifanyika dhifa za kitaifa, linalojulikana kama Temple of Heaven.

Pamoja na suala la Iran, serikali ya Trump inatarajia kuanzisha Bodi ya Biashara na China itakayoshughulikia tofauti baina ya mataifa hayo mawili.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW