1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Emmanuel Macron aanza ziara nchini Madagascar

23 Aprili 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameanza ziara ya siku mbili nchini Madagascar kuimarisha mahusiano na nchi hiyo.

Rais Emmanuel Marcon na mkewe Brigitte
Rais Emmanuel Marcon na mkewe BrigittePicha: Thomas Padilla/Pool via REUTERS

Ziara hiyo ya Macron inalenga kuimarisha mahusiano kati ya nchi hizo mbili pamoja na kuendelea kuimarisha uwepo wa Ufaransa katika eneo hilo la Bahari ya Hindi, licha ya kuwepo mivutano inayoendelea ya enzi ya ukoloni.

Ni ziara ya kwanza rasmi ya kiongozi wa Ufaransa nchini Madagascar tangu ile iliyowahi kufanywa mwaka 2005 na Jacques Chirac.

Rais Macron aliyeandamana kwenye ziara hiyo na mkewe Brigitte atakuwa na mikutano na Rais Andry Rajoelina na viongozi wa kibiashara mjini Antananarivo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW