1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Herzog kuzingatia nchi kwanza kuhusu ombi la Netanyahu

1 Desemba 2025

Rais wa Israel Isaac Herzog, amesema atazingatia tu masilahi bora ya Israel atakapoamua kuhusu ombi la Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu la kutaka apate msamaha wa rais kuhusiana na mashtaka ya ufisadi dhidi yake.

Israel Tel Aviv 2025 | Rais wa Israel Isaac Herzog akitoa hotuba
Rais wa Israel Isaac Herzog asema atazingatia zaidi masilahi muhimu ya nchi atakapoamua kuhusu ombi la Netanyahu kutaka msamaha wa rais kwa mashtaka ya ufisadi dhidi yakePicha: Jack Guez/AFP

Kwenye taarifa yake, Herzog amesema suala hilo litazingatiwa kwa njia sahihi kabisa, na kwamba ataongozwa na masilahu muhimu ya nchi ya Israel atakapotoa uamuzi.

Netanyahu alitangaza siku ya Jumapili kwamba amewasilisha rasmi ombi la kutaka msamaha wa rais akisema kesi hizo zinazidi kuigawa Israel.

Rais wa Marekani Donald Trump pia alimuandikia barua Rais Herzog akimsihi amsamehe Netanyahu, ambaye mara kwa mara amekanusha mashtaka dhidi yake.

Netanyahu na mkewe wanakabiliwa na mashtaka ya kukubali bidhaa za thamani ya zaidi ya dola 260,000 kama rushwa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW