1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais John Pombe Magufuli ameapishwa kwa muhula wa pili

Yusra Buwayhid
5 Novemba 2020

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ameapishwa leo kuendelea na wadhifa huo kwa muhula wa pili madarakani, kufuatia uchaguzi mkuu wa Oktoba 28.

Tansania Vereidigung Präsident John Magufuli
Picha: AP Photo/picture alliance

John Pombe Magufuli ameapishwa kufuatia ushindi wake kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 28.

Upinzani hata hivyo unadaia uchaguzi huwo ulikuwa na dosari, na udanganganyifu. Halikadhalika umeyakataa matokeo ya uchaguzi huo, na kutaka urudiwe tena, tume ya uchaguzi ivunjwe pamoja na kuitisha maandamano yasiyo na kikomo.

Soma pia: Magufuli aahidi kufanya kazi ya upinzani

Usalama uliimarishwa kabla ya kuanza kwa hafla hiyo ya kuapishwa Magufuli, na viongozi wa vyama viwili vikuu vya upinzani vya Tanzania, ACT-Wazalendo na CHADEMA, walishtakiwa kwa kuandaa maandamano kinyume cha sheria.

Magufuli aapishwa kwa muhula wa pili

This browser does not support the audio element.

Mwishoni mwa wiki Rais Magufuli alisema hatowania muhula mwengine wa uongozi, huku kukiwa na wasiwasi kwamba chama tawala CCM, ambacho kimeshinda karibu viti vyote bungeni, huwenda kikajaribu kuongeza kikomo cha mihula miwili ya urais.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW