Rais Macron wa Ufaransa yuko ziarani nchini India
17 Februari 2026
Matangazo
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameanza ziara yake ya siku tatu leo nchini India ambako atakutana na waziri mkuu wa India Narendra Modi.
Ziara hiyo inajikita kutazama zaidi ushirikiano katika sekta ya teknolojia ya akili mnemba pamoja na uwezekano wa kufikia mpango wa mabilioni ya dola wa kuiuzia India ndege za kivita.
Ufaransa inatafuta kutanua ushirikiano wake wa kijeshi na New Delhi, huku mazungumzo yakitarajiwa kuhusu uwezekano wa kufikiwa mkataba wa mauzo ya ndege 114 za kivita za Kifaransa aina ya Dassault Rafale.
Waziri mkuu Modi amesema anaamini mazungumzo yake na rais Macron atakayekutana nae baade leo yataimarisha zaidi ushirikiano wa mataifa yao mawili.