1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Mahmoud Abbas ziarani Marekani

23 Aprili 2008

-

WASHINGTON

Rais wa Palestina Mahmoud Abbas yuko nchini Marekani kwa ajili ya kuwa na mazungumzo na rais Goerge W Bush pamoja na maafisa wengine wa ngazi za juu nchini humo.Rais Mahmoud Abbas ambaye aliwasili hapo jana mjini Washington amepangiwa hii leo asubuhi kukutana na wabunge na baadae kuwa na baadae atakuwa na mkutano na waziri wa mambo ya nje Condolezza Rice.Rais Goerge Bush ambaye alianzisha juhudi mpya za kutia msukumo makubaliano ya amani kati ya Israel na Palestina atajadiliana hapo kesho na rais Abbas juu ya maendeleo katika suala hilo.