Rais Marcron aitembelea Syria
7 Julai 2026
Matangazo
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron yuko ziarani nchini Syria. Macron aliwasili Damascus jana Jumatatu kwa ziara ya kwanza ya mkuu wa nchi wa Ulaya Magharibi tangu mamlaka mpya ya Syria ilipochukua madaraka.
Macron alisema amekwenda Syria kuthibitisha tena kujitolea kwa Ufaransa kwa watu wa Syria, kwa Syria huru iliyoungana katika utofauti wake na yenye amani na majirani zake.
Macron na rais wa mpiti wa Syria Ahmed al-Sharaa waliutembelea msikiti maarufu wa Umayyad wa Damascus baada ya chakula cha jioni kabla mikutano rasmi inayotarajiwa kufanyika leo Jumanne.
Macron anatarajiwa kuondoka leo kurejea nyumbani Ufaransa.