1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Sall wa Senegal akabiliwa na mbinyo kuhusu uchaguzi

15 Februari 2024

Rais wa Senegal Macky Sall amekutana na baraza lake la mawaziri jana, wakati akizidi kukabiliwa na shinikizo la ndani na la kimataifa kurejea katika kalenda ya uchaguzi uliocheleweshwa na kutatua mzozo mkubwa wa kisiasa.

Senegal I Uchaguzi -  Macky Sall
Rais Macky Sall akihudhuria mkutano wa majadiliano ya kitaifa unaolenga kutuliza hali kuelekea uchaguzi mkuu.Picha: Ngouda Dione/File Photo/REUTERS

Rais wa Senegal Macky Sall amekutana na baraza lake la mawaziri jana, wakati akizidi kukabiliwa na shinikizo la ndani na la kimataifa la kurejea katika kalenda ya uchaguzi uliocheleweshwa na kutatua mzozo mkubwa wa kisiasa.

Taarifa iliyotolewa baada ya mkutano wa rais na baraza lake la mawaziri, ilizungumzia kidogo juu ya mzozo wa kisiasa unaoendelea. Ofisi ya rais, imechapisha video kwenye mitandao ya kijamii ikihimiza mazungumzo ya wazi ya kitaifa kabla ya uchaguzi.

Soma pia: Uchumi wa Senegal kuzorota kutokana na mkwamo wa kisiasa

Marekani, Ufaransa na Umoja wa Mataifa zimeunga mkono matakwa ya Wasenegali ya kutaka upigaji kura ufanyike haraka iwezekanavyo katika uchaguzi uliokuwa ufanyike Februari 25.

Kumekuwa na hofu kwamba mvutano huo unaweza kuenea na kusababisha ghasia zaidi. Watu watatu wameuawa katika maandamano, tangu Rais Sall alipotangaza kuchelewesha uchaguzi hadi Februari 25 Desemba.