1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Samia apokea ripoti ya tume ya kuchunguza mzozo, Ngorongoro

13 Machi 2026

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepokea ripoti za tume zilizoundwa kuchunguza mgogoro uliotokana na kuwahamisha wakazi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro. Ripoti hizo zimebainisha kasoro kadhaa.

Tansania Dodoma 2026 | Übergabe des Kommissionsberichts zur Landnutzung im Ngorongoro-Schutzgebiet an Präsidentin Hassan
Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Katibu Mkuu Mstaafu, Mhandisi Musa Iyombe akimkabidhi Taarifa ya Tume hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Ikulu ya Chamwino Mkoani DodomaPicha: Najjat Omar/DW

Rais Samia Suluhu  alipokea ripoti mbili za tume zilizoundwa kuchunguza mgogoro wa hifadhi ya Ngorongoro. Ripoti hizo zimebaini kuwa wananchi hawakushirikishwa vya kutosha, kukosekana kwa sheria na sera zinazoongoza mpango wa kuwahamisha wakazi hao, na mpango wa kuwahamisha ukitumia zaidi ushawishi badala ya utashi.

Hata hivyo Rais akiwa jijini Dodoma, alisema serikali itaendelea na mpango wa kuwahamisha wakazi hao kwa kutumia mfumo unaosisitiza hiari ya wananchi na ushirikishwaji mpana wa jamii.

Mgogoro wa hifadhi ya Ngorongoro ulisikika kwa mara ya kwanza mwaka 2022 baada ya wakazi wanaoishi eneo la hifadhi ya Ngorongoro wengi wao wakiwa ni jamii ya wamaasai, wakilalamika kuondolewa katika eneo ambamo wameishi kwa miaka mingi.

Baada ya baadhi ya wakazi kuhamishwa katika utaratibu uliotajwa kuwa wa hiari, baadhi ya wakazi wa eneo hilo walihamia Tanga, Msomera lakini kukawepo malalamiko zaidi ya uvunjwaji wa haki za binadamu ikiwamo kuhamishwa kwa nguvu.

Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Katibu Mkuu Mstaafu, Mhandisi Musa Iyombe Picha: Najjat Omar/DW

Mkazi wa Ngorongoro, Kijiji cha Pololek, Kasale Mwaana, ameiambia DW, ripoti za tume zimepigilia muhuri kondolewa kwa wamasai Ngorongoro.

Desemba 2024, Rais Samia Suluhu Hassan aliunda tume mbili  ya Dk Gerald Ndika na ya Jaji Musa Iyombe kuchunguza mgogoro huo uliovutia wanaharakati wa mazingira wa kimataifa na watetezi wa haki za binadamu.

Mkazi mwingine wa  Ngorongoro, Nain Tipap, anasema, ripoti hiyo haijagusa maslahi ya wananchi.

Ripoti hizo zimebainisha kuwa mpango wa awali wa kuwahamisha wakazi wa Ngorongoro haukufanikiwa kwani kaya zilizofanikiwa kuhama ni 1678, kati ya kaya 23,000 zinazoishi Ngorongoro huku akibainisha zaidi kuwa kuna nyumba  1559 zilizojengwa Msomera Tanga, ambazo hazijapata wakaazi. 

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW