Rais Samia Suluhu Hassan afanya ziara nchini Urusi
3 Juni 2026
Katika mkutano ulioonyeshwa moja kwa moja kwenye televisheni uliofanyika Kremlin, Samia alielezea ziara yake nchini humo kuwa ya kihistoria.
Kwa upande wake, Putin alisema amefurahi kumuona Samia nchini Urusi na akatoa wito kwa nchi hizo mbili kuongeza biashara kati yao.
Kwa sasa, biashara kati ya Tanzania na Urusi inakadiriwa kufikia zaidi ya dola milioni 307 za Marekani kwa mwaka. Mradi pekee wa pamoja wenye umuhimu mkubwa ni mgodi wa urani unaopangwa kujengwa, ambao umekuwa ukisubiri kutekelezwa kwa zaidi ya muongo mmoja.
Profesa wa zamani wa siasa kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, alieyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina, amesema Urusi inaweza kufaidika na uungwaji mkono wa Tanzania, hata kama ni kwa Tanzania kujizuia kupiga kura katika kura muhimu za Umoja wa Mataifa kuhusu vita vya Ukraine.