1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Trump apanga kulihutubia taifa Jumanne

23 Februari 2026

Masuala ya siasa za ndani yatarajiwa kwenye hotuba ya Trump, japo vitisho vyake kwa Iran linaweza kuwa suala litakalogubika hotuba hiyo

Wamarekani wasubiri kuona hotuba ya rais Donald Trump itatowa mwelekeo gani kwa taifa
Wamarekani wasubiri kuona hotuba ya rais Donald Trump itatowa mwelekeo gani kwa taifaPicha: Kevin Dietsch/Getty Images

 Rais Donald Trump wa Marekani anatarajiwa kutowa hotuba yake kwa taifa kesho Jumanne, ambayo huenda ikawa kipimo cha ujumbe unaotaka kufikishwa na chama chake cha  Republican kwa wapiga kura wa nchi hiyo kuelekea uchaguzi wa katikati ya muhula.

Mwelekeo wa hotuba ya Trump ndio utakaoweza kuamuwa ikiwa chama hicho kitaungwa mkono kudhibiti bunge na baraza la Seneti nchini Marekani.Trump aongeza ushuru kimataifa kutoka asilimia 10 hadi 15

Kura za maoni zinaonesha majimbo mengi nchini humo yamepoteza imani na namna rais Trump alivyosimamia serikali  katika muhula wake huu wa kwanza tangu aliporejea tena madarakani.

Kwa kiasi kikubwa hotuba ya Trump kwa taifa inatarajiwa kujikita kwenye masuala ya ndani ya Marekani lakini  vitisho vya kuishambulia Iran kutokana na mpango wake wa Nyuklia, ambavyo amekuwa akizidi kuvitowa, huenda ni suala linaweza kuigubika hotuba hiyo hapo kesho.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW