Rais Trump kutoa Hotuba ya Hali ya Taifa
24 Februari 2026
Matangazo
Trump atahutubia mabaraza yote mawili ya Bunge huko Washington, na hotuba hiyo huenda ikatoa mwangaza wa tathmini ya Trump kuhusu utendaji wa utawala wake kabla ya uchaguzi wa katikati ya muhula mwezi Novemba.
Anatoa hotuba hiyo siku chache baada ya Mahakama Kuu kufuta baadhi ya ushuru ambao ni sera muhimu kwa kiongozi huyo, na ambayo imewaacha njia panda washirika wengi wa kibiashara duniani.
Hotuba hii ya Hali ya Taifa pia inatolewa katika mwaka muhimu kwa Marekani, ambayo inaadhimisha miaka 250 tangu Azimio la Uhuru Julai 4, 1776.