Rais wa Afghanistan ziarani nchini Ujerumani
18 Machi 2007Matangazo
Düsseldorf:
Rais Hamid Karzai wa Afghanistan akianza ziara rasmi nchini Ujerumani,amesifu mchango wa jeshi la Ujerumani Bundeswehr katika vikosi vya kuzlinda amani nchini mwake.Rais Karzai amesema mjini Düsseldorf, kwa namna hiyo,hali ya usalama itaimarika nchini Afghanistan na barani Ulaya pia.Kesho rais huyo wa Afghanistan atakwenda Berlin kwa mazungumzo pamoja na kansela Angela Merkel.