1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaColombia

Rais wa Colombia Petro apinga vitisho vya Trump

5 Januari 2026

Rais wa Colombia Gustavo Petro amevipinga vitisho vinavyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani ambaye pia anamshutumu kiongozi huyo kwa kufanya biashara haramu ya dawa za kulevya.

Marekani Colombia | Picha ya pamoja ya maraisa Gustavo Petro wa Colombia na Donald Trump wa Marekani
Rais Donald Trump wa Marekani amemuonya Rais wa Colombia Gustavo Petro, huku akisema huenda akaishambulia kama alivyofanya Venezuela kutokana na shutuma za madawa ya kulevyaPicha: Federico Parra/Andrew Caballero-Reynolds/AFP

Petro kupitia mtandao wa X amekanusha vikali madai hayo akisema jina lake halijaonekana kwenye rekodi za mahakama na amemtaka Trump aache kumkashifu.

Jana Jumapili, Trump aliwaambia waandishi wa habari kwamba atachukua hatua za kijeshi dhidi ya Colombia, baada ya kuishambulia Venezuela na kumuondoa Rais wake Nicolas Maduro kwa shutuma kama hizo za biashara ya dawa za kulevya.

"Kwa sasa tuna jirani mwenye hali mbaya. Sio jirani, lakini yuko karibu na jirani yetu. Inakera. Colombia ina hali mbaya pia, ikiongozwa na mtu asiyejitambua anayependa kutengeneza na kuuza dawa aina ya cocaine nchini Marekani. Lakini hataendelea kufanya hivyo kwa muda mrefu. Ache niwaambie," alisema Trump.

Petro aidha amekosoa vikali hatua ya kijeshi ya utawala wa Trump nchini Venezuela na kuishutumu Washington kwa kumteka nyara Maduro "nje ya msingi wa kisheria."

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW