Rais wa Iran alitaka taifa kushikamana badala ya kuandamana
31 Desemba 2025
Matangazo
Mwito wake umefuatia wimbi kubwa la maandamano ya umma yanayoshuhudiwa nchini humo tangu siku ya Jumapili kutokana na hali mbaya ya uchumi.
Rais Pezeshkian amesema taifa hilo linapitia mambo mengi ikiwemo shinikizo kutoa kwa maadui wa Jamhuri hiyo ya kiislamu, akisisitiza kuwa huu ni wakati wa raia kuungana kukabiliana na hali iliyopo na sio kuandamana.
Hata hivyo baadhi ya waandamanaji bado wanailaumu serikali kwa hali mbaya ya kiuchumi wakisema sera zake ndio sababu kuu ya mdororo wa uchumi katika taifa hilo lililo tajiri kwa mafuta na gesi.
Iran inahusisha maandamano ya siku nne nchini humo na njama za nchi za kigeni zinazolenga kuisukuma nchi hiyo katika machafuko na ukosefu wa utulivu.